015-Kutoa Zakaah: Kutoa Panapowajibika

 

Kutoa Zakaah: Kutoa Panapowajibika

 

Alhidaaya.com

 

 

Inawajibika kuitoa Zakaah wakati wake unapowadia, na haijuzu kuichelewesha isipokuwa kwa dharura inayokubalika.

 

Kutoka kwa Bibi ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema kuwa; Nabiy (Swalla Alaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

"Haichanganyiki mali pamoja na Zakaah isipokuwa itaiangamiza", na katika riwaya nyingine;

 

"Inakuwa ishakuwajibikia katika mali yako kuitolea Zakaah, kisha usiitoe, kwa hivyo (mali ya) haramu (isiyotolewa Zakaah) inaiangamiza (mali ya) halali". [Ash-Shaafi’iy na Al-Bukhaariy katika 'At-Taariykh']

Share