031-Kutoa Zakaah: Watu Wema

 

Kutoa Zakaah: Watu Wema

 

Alhidaaya.com

 

 

Zakaah anapewa Muislam anayeistahiki akiwa Muislam huyo ni mtu mwema au mtu asi, isipokuwa mtu asi hapewi katika mali ya Zakaah ikiwa itajulikana kwa uhakika kuwa atakuja kuitumia mali hiyo katika kuuendeleza uasi wake. Ikijulikana kwa uhakika kuwa ataitumia mali hiyo katika kumuasi Allaah, basi mtu huyo atanyimwa, ama ikiwa hayajulikani hayo, au ikijulikana kuwa ataitumia mali hiyo katika shida zake, basi hapo atapewa.

 

Hata hivyo ni bora kwa mtoaji Zakaah aihusishe mali hiyo kwa kuwapa watu wema au maulamaa wanaostahiki wanaoifayia kazi elimu yao, kwani Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

"Walisheni chakula chenu wacha wa Allaah na mnaowajuwa katika walioamini (kweli)". [Ahmad]

 

Anasema Ibn Taymiyah:

 

"Asiyeswali hapewi katika mali ya Zakaah mpaka pale atakapotubu akawa anaswali."

 

Anasema Sayyid Saabiq:

 

"Katika kundi hilo wanaingia pia wale wanaomuasi Allaah bila kujali wala kuona haya, na kuendelea kuzama katika maasi huku nyoyo zao zikiwa ziAsh-Shaafi’iysidika na dhamiri zao zimekwisha haribika".

 

Hawa hawapewi katika mali ya Zakaah isipokuwa kama Zakaah hiyo itawasaidia katika kuwaongoza mwongozo ulio sahihi au itawasaidia katika kutoka hali yao hiyo.

 

Share