Ameombewa Du’aa Na Majirani Makafiri Wakati Wa Kukata Roho, Je Itaathiri Imani Yake?

SWALI:

 

Assalam Aleikum ndugu waislam, natoa shukrani zangu kwa kazi yenu nzuri mwenyezi mungu atawaji mema.Mimi nina swali linanipa dhiki sana nalo ni hili, mimi nilikuwa nimeolewa na mume wangu wa kwanza ambae alifariki miaka mitatu ya liopita na katika kifo chake kulikuwa hakuna mtu bali ni mimi na yeye hakuwa mgonjwa aliamka na pumu siku hiyo niliona ni pumu zake za kawaida lakini sivo nilivodhani ilikuwa ni mauti,nilipiga kelele jirani yangu tunaishi nyumba moja akatokea na mume wake walipoona ile hali wakaamua kuomba kwa dini yao kwani walijua yuko kwenye sakaratmaut nahawakunijulisha chochote kama mume wangu yuwatuacha ilinimpe maneno mema ingawa nilikua nikisema kwa kelele laillailallah bali haikuwa inavotakikana.Naomba munifamishe ikiwa nilimkosea aliyefariki kutompa shahada na wale jirani ambao siisilamu yale maombi yao yatamtia aliyefariki dhambini.Shukran


 

JIBU: 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho. 

Shukrani kwa swali lako kuhusu kubabaika kwako wakati mumeo anakata roho.

Hakika hakuna kitakachomdhuru aliyefariki ikiwa hakupata taathira yoyote ile wakati majirani zako wasiokuwa Waislamu walikuwa wanaomba. Ataathirka tu mbele ya Allaah Aliyetukuka ikiwa mumeo aliweza kuyashika na kutamka yale yaliyokuwa yakisemwa na hao majirani zake. 

Sisi kama Waislamu tunatakiwa tuwe makini wakati jamaa zetu wapendwa ni wagonjwa au wanakata roho ili katika utulivu huo tuweze kuwaelekeza. 

Tunaomba kuwa shahada uliyokuwa ukiitoa kwa mayowe japokuwa inatakiwa iwe polepole imesibu kumfikia mumeo naye akatamka.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share