Anaweza Kuwamiliki Majini Na Kuwaamrisha Atakavyo?

 

Anaweza Kuwamiliki Majini Na Kuwaamrisha Atakavyo?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Assalam alikum warhmatu Allaahu Taala wabarakatuh.

 

Kuna kitu chochote binadamu anaweza kufanya ili majini wake wamuogope na kumfanyia vitu anavyovitaka? Ahsante

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

Hilo linawezekana kwani Allaah Aliyetukuka Amewapatia uwezo wanaadamu juu ya viumbe wengine vyote.

 

Hata hivyo, utumiaji huo unakuwa ni wa pande mbili, yaani nipa nikupe. Yeye atakutumikia nawe ni lazima ufuate yale yake ayatakayo ambayo yanamuingiza mmoja wetu katika ushirikina na ukafiri.

 

Hivyo, pamoja na kuwezekana jambo hilo, lakini si jambo ambalo Muislamu anapaswa kulifanya au kujifunza. Na haifai kushirikiana na watu wanaojihusisha na mambo kama hayo.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share