Al-Lajnah Ad-Daaimah: Maulidi: Hukmu Ya Kusherehekea Maulidi Ya Nabiy ﷺ

 

Hukmu Ya Kusherehekea Maulidi Ya Nabiy (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam) Katika Mwezi Wa Rabiy’ul-Awwal Kwa Ajili Ya Kumuadhimisha

 

Al-Lajnah Ad-Daa'imah

www.alhidaaya.com

 

SWALI:

 

Nini hukmu ya kusherehekea mawlid ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika mwezi wa Rabiy’ul Awwal kwa ajili ya kumuadhimisha?

 

 

JIBU:

 

Kumuadhimisha Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumheshimu ni kwa  kuamini kila alilokuja nalo kutoka kwa Allaah, na kufuata Shariy’ah Yake, ki-‘Aqiydah, na kwa kauli na kwa matendo na tabia, na kuacha bid’ah katika Dini.

Na katika mambo ya bid’ah ni kusherehekea Mawlid Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

 

Wa biLLaahit-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyinaa Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

[Fatwa (3257) – Al-Lajnah Ad-Daaimah]

 

 

 

Share