Shaykh Fawzaan: Nani Kasema Mnyoa Ndevu Hawezi Kuingia Motoni?

 

Nani Kasema Mnyoa Ndevu Hawezi Kuingia Motoni?

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Nimejadiliana mimi na ndugu zangu kuhusu ndevu. Wakaniingiza ndani ya utata na kunambia kuwa ndevu sio faradhi wala wajibu. Lau ingelikuwa ni wajibu kwa mfano mwenye kufanya hivyo angelikuwa anaingia Motoni pamoja na kuwa ananyoa ndevu zake.

 

 

JIBU:

 

Ni kipi kinachompa matumaini ya kutoingia Motoni? Mtenda madhambi anaingia Motoni. Huyu anasema kwamba anayenyoa ndevu zake hawezi kuingia Motoni? Ni mwenye kutishiwa na kukhofiwa kuingia Motoni na kupewa adhabu na tunajikinga kwa Allaah. Kila mwenye kuasi basi ni mwenye kukhofiwa juu yake adhabu. Ni nani aliyemwambia kwamba mwenye kunyoa ndevu hawezi kuingia Motoni?

 

[Shaykh Swaalih Al-Fawzaan]

 

www.alfawzan.af.org.sa/node/13054

 

 

Share