01-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Twahaarah: Mlango Wa Maji

بُلُوغُ الْمَرام بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتابُ الطَّهارَة

Kitabu Cha Twahaarah

 

بَابُ الْمِياهِ

01-Mlango Wa Maji

 

 

 

 

1.

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏فِي اَلْبَحْرِ:   ‏{ هُوَ اَلطُّهُورُ مَاؤُهُ، اَلْحِلُّ مَيْتَتُهُ } أَخْرَجَهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَابْنُ أَبِي شَيْبَةَ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ وَاَلتِّرْمِذِيُّ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah[1] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuhusu bahari: “Maji yake yanatwaharisha, na maiti wake ni halaal (kuliwa).” [Imetolewa na Al-Arba’ah: Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na Ibn Maajah  na Ibn Abiy Shaybah na tamshi la Hadiyth hii ni lake Ibn Khuzaymah akaisahihisha na At-Tirmidhiy]

 

 

2.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم: {إِنَّ اَلْمَاءَ طَهُورٌ لَا يُنَجِّسُهُ شَيْءٌ)) أَخْرَجَهُ اَلثَّلَاثَةُ  ‏ وَصَحَّحَهُ أَحْمَدُ   ‏

Kutoka kwa Sa’iyd Al-Khudriyy[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ)  amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  amesema: “Hakika maji ni masafi[3], hayanajisiwi na kitu.”  [Imetolewa na Ath-Thalaathah: Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy  na akaisahihisha Ahmad] 

 

 

3.

وَعَنْ أَبِي أُمَامَةَ اَلْبَاهِلِيِّ رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ صلى الله عليه وسلم: {إِنَّ اَلْمَاءَ لَا يُنَجِّسُهُ شَيْءٌ، إِلَّا مَا غَلَبَ عَلَى رِيحِهِ وَطَعْمِهِ، وَلَوْنِهِ} أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَاجَهْ ‏ وَضَعَّفَهُ أَبُو حَاتِمٍ

Kutoka kwa Abuu Umaamah Al-Baahiliyy[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ)  amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  amesema: “Hakika maji hayanajisiwi na chochote isipokuwa kinachozidi harufu yake, ladha yake na rangi.”   [Imetolewa na Ibn Maajah na Abuu Haatim akaidhoofisha]

Aliyepokea Al-Bayhaqiyy: “Maji ni yenye kutwahirisha isipokuwa yakiingia najsi na kuyabadilisha harufu, ladha au rangi[5] yake.”

 

 

4.

وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: {إِذَا كَانَ اَلْمَاءَ قُلَّتَيْنِ لَمْ يَحْمِلْ اَلْخَبَثَ}

 

 وَفِي لَفْظٍ: {لَمْ يَنْجُسْ}   أَخْرَجَهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ‏ وَابْنُ حِبَّانَ 

Kutoka kwa ‘Abdullaahi bin ‘Umar[6] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا)  amesema:  Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  amesema: “Pindi maji yakiwa qullatayn[7] (viriba au mitungi miwili) huwa hayachukui uchafu.”

 

Na katika tamshi: “Haifanyi kuwa najisi.” [Imetolewa na Al-Arba’ah na ameisahihisha Ibn Khuzaymah na Ibn Maajah]

 

 

5.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم:  { لَا يَغْتَسِلُ أَحَدُكُمْ فِي اَلْمَاءِ اَلدَّائِمِ وَهُوَ جُنُبٌ}  أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ 

وَلِلْبُخَارِيِّ: {لَا يَبُولَنَّ أَحَدُكُمْ فِي اَلْمَاءِ اَلدَّائِمِ اَلَّذِي لَا يَجْرِي، ثُمَّ يَغْتَسِلُ فِيه} ‏
وَلِمُسْلِمٍ: {مِنْهُ}‏
وَلِأَبِي دَاوُدَ: {وَلَا يَغْتَسِلُ فِيهِ مِنْ اَلْجَنَابَةِ}

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ)  amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asioge mmoja wenu katika maji yaliyotuwama ilhali ana janaba.” [Imetolewa na Muslim]

 

 Na katika Al-Bukhaariy: “Asikojoe mmoja wenu katika maji yaliyotuwama ambayo hayaendi kisha akaoga ndani yake[8].” 

 

Na katika riwaayah nyengine ya Muslim: “Kutoka humo” (yaani kutoka kwenye maji hayo).

 

Na kwa Abuu Daawuwd: “Mtu asioge humo janaba.”  

 

 

6.

وَعَنْ رَجُلٍ صَحِبَ اَلنَّبِيَّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏"أَنْ تَغْتَسِلَ اَلْمَرْأَةُ بِفَضْلِ اَلرَّجُلِ، أَوْ اَلرَّجُلُ بِفَضْلِ اَلْمَرْأَةِ، وَلْيَغْتَرِفَا جَمِيعًا  .أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ.‏ وَالنَّسَائِيُّ، وَإِسْنَادُهُ صَحِيحٌ.‏

Mtu mmoja[9] aliyesuhubiana na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alisema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza mwanamke kuoga mabaki ya maji ya mwanamume  na mwanamume kuoga mabaki ya maji ya mwanamke, wachote pamoja.”

[Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na Isnaad yake ni Swahiyh]

 

 

 

7.

عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏كَانَ يَغْتَسِلُ بِفَضْلِ مَيْمُونَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا.   أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ .‏

 

وَلِأَصْحَابِ "اَلسُّنَنِ:  اِغْتَسَلَ بَعْضُ أَزْوَاجِ اَلنَّبِيِّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏فِي جَفْنَةٍ، فَجَاءَ لِيَغْتَسِلَ مِنْهَا ، فَقَالَتْ لَهُ: إِنِّي كُنْتُ جُنُبًا، فَقَالَ: {إِنَّ اَلْمَاءَ لَا يُجْنِبُ} وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ‏

 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas[10] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا)  kwamba Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  alikuwa akioga kwa maji yaliyoacha na Maymuwnah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا).” [Imetolewa na Muslim]

 

Na katika mapokezi ya Aswhaab As-Sunan]:

“Mmoja katika ya wake wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  alioga kwenye beseni kisha Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaja kuoga katika chombo hicho, huyo mkewe[11] akamwambia: “Mimi nilikuwa na janaba.”  Akasema: “Hakika maji hayapati janaba.”  [Ameisahihisha At-Tirmidhiy na Ibn Khuzaymah]

 

 

8.

 وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم: {طَهُورُ إِنَاءِ أَحَدِكُمْ إِذْ وَلَغَ فِيهِ اَلْكَلْبُ أَنْ يَغْسِلَهُ سَبْعَ مَرَّاتٍ، أُولَاهُنَّ بِالتُّرَابِ}  أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ.‏

وَفِي لَفْظٍ لَهُ: { فَلْيُرِقْهُ }‏

وَلِلتِّرْمِذِيِّ: { أُخْرَاهُنَّ، أَوْ أُولَاهُنَّ بِالتُّرَابِ }‏ .‏

 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kutwaharisha chombo cha mmoja wenu ikiwa kimelambwa na mbwa, ni ki kukiosha mara saba[12].” 

[Imetolewa na Muslim].

 

Tamshi jengine la Muslim: “Basi amwage.”

Na katika riwaayah ya Imaam At-Tirmidhiy: “Kwanza au mwisho wake kwa mchanga.” 

 

 

9.

وَعَنْ أَبِي قَتَادَةَ ‏ رضى الله عنه  أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ ‏فِي اَلْهِرَّةِ‏: { إِنَّهَا لَيْسَتْ بِنَجَسٍ، إِنَّمَا هِيَ مِنْ اَلطَّوَّافِينَ عَلَيْكُمْ } أَخْرَجَهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ.‏ وَابْنُ خُزَيْمَةَ‏.‏

 

Kutoka kwa Abuu Qataadah[13] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuhusu paka: “Huyo si najsi bali ni mmoja wa wananchanganyika nanyi.”  [Imetolewa na Al-Arba’ah: Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na Ibn Maajah  na ameisahihisha At-Tirmidhiy na Ibn Khuzaymah]

 

 

10.

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: { جَاءَ أَعْرَابِيٌّ فَبَالَ فِي طَائِفَةِ اَلْمَسْجِدِ، فَزَجَرَهُ اَلنَّاسُ، فَنَهَاهُمْ اَلنَّبِيُّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏فَلَمَّا قَضَى بَوْلَهُ أَمَرَ اَلنَّبِيُّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏بِذَنُوبٍ مِنْ مَاءٍ، فَأُهْرِيقَ عَلَيْهِ}.‏  مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ.‏

 

Kutoka kwa Anas bin Maalik[14] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Bedui mmoja alikuja akakojoa katika pembe ya Msikiti, watu wakamkemea Lakini Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  akawakataza.  Alipomaliza mkojo wake, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  akaamrisha iletwe ndoo ya maji, ikamwagiwa[15] juu yake (huo mkojo). [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

11.

وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{ أُحِلَّتْ لَنَا مَيْتَتَانِ وَدَمَانِ، فَأَمَّا الْمَيْتَتَانِ: فَالْجَرَادُ وَالْحُوتُ، وَأَمَّا الدَّمَانُ: فَالطِّحَالُ وَالْكَبِدُ } أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَفِيهِ ضَعْفٌ

 

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا)  kwamba Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  amesema: “Tumehalalishiwa maiti za aina bili na damu za aina mbili. Ama maiti mbili ni nzige na samaki ، na ama damu mbili  ni bandama na ini.” [Imetolewa na Ahmad na Ibn Maajah na Hadiyth hii ina yaliyo dhaifu]

 

 

12.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏} إِذَا وَقَعَ اَلذُّبَابُ فِي شَرَابِ أَحَدِكُمْ فَلْيَغْمِسْهُ، ثُمَّ لِيَنْزِعْهُ، فَإِنَّ فِي أَحَدِ جَنَاحَيْهِ دَاءً، وَفِي اَلْآخَرِ شِفَاءً } أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ.‏

 

وَأَبُو دَاوُدَ ، وَزَادَ: { وَإِنَّهُ يَتَّقِي بِجَنَاحِهِ اَلَّذِي فِيهِ اَلدَّاءُ }

 

Kutoka kwa Abuu  Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  amesema: “Pindi nzi akiangukia katika kinywaji cha mmoja wenu, basi amazmishe kisha amtoe , kwani kuna ugonjwa katika moja ya bawa lake na tiba katika bawa jengine[16].”  [Imetolewa na Al-Bukhaariy ]

 

Na Abuu Daawuwd ambaye aliongeza:

 

“Kwani yeye (inzi) huangulikia kwa bawa lake lenye ugonjwa.”

 

 

13.

عَنْ أَبِي وَاقِدٍ اَللَّيْثِيِّ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ اَلنَّبِيُّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{ مَا قُطِعَ مِنْ اَلْبَهِيمَةِ ‏وَهِيَ حَيَّةٌ‏ فَهُوَ مَيِّتٌ } أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ، وَاللَّفْظُ لَهُ.‏

 

Kutoka kwa Abuu Waaqid Al-Laythiyy[17] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kwamba Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kilichokatwa kutoka kwa mnyama aliye hai basi hicho ni maiti.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na ameipa daraja ya Hasan na tamashi hili ni lake]

 

 

 

 

[1] Abuu Hurayrah: Jina lake halisi ni ni ‘Abdullaah au ‘Abdur-Rahmaan bin Sakhr Ad-Daws, mmoja wa Swahaba wakubwa wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na alipokea Hadiyth nyingi kuliko wote. Zaidi ya watu 800 walipokea kutoka kwake. Alisilimu katika mwaka wa Khaybar (7H) na akawa karibu na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) mpaka Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipofariki. Akateuliwa kuwa Mufti (Mwanazuoni wa hukumu za Kiislaam) wakati wa Ukhalifa wa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) na baadaye akawa gavana wa Madiynah wakati wa utawala wa Marwaan bin Al-Hakam. Alifariki mwaka 59 H na akazikwa Al-Baqi’.

 

[2] Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy: Jina lake ni Sa’d bin Maalik bin Sinan Al-Khazraj Al-Answaar. Alikuwa miongoni mwa Swahaba wasomi. Alipokea Hadiyth nyingi, na alitoa rai za kidini kwa muda fulani. Alifariki mwanzoni mwa mwaka wa 74H akiwa na umri wa miaka 86.

 

[3] Imepokewa na Ahmad, At-Tirmidhiy, na Abuu Daawud kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alisema maneno hayo katika kujibu swali kuhusu kisima cha Buda’a, kilicho karibu na Madiynah, na daima kilijaa uchafu. Kilikuwa kwenye eneo lililo chini, na maji ya mvua yalikuwa yanapeleka uchafu na takataka kisimani. Maneno haya bila shaka yanakihusu.

 

[4] Abuu Umaamah Al-Baahiliy: Jina lake halisi ni Suday bin Ajlaan akiwa ni mmoja wa Swahaba waliopokea Hadiyth nyingi. Aliishi Misri, kisha akahamia Hims (sasa iko Syria), na akafia kule akiwa na umri wa miaka 81 au 86.

 

[5] Baadhi ya watu wamehoji kwamba, maji yanaweza kupunguka au kuongezeka wingi wake ikiwa huo uchafu au taka zitabadili moja ya sifa zake hizo tatu (rangi, harufu na ladha), na hapo maji yatanajisika. Lakini maoni sahihi katika maudhui haya ni kuwa, iwapo maji yako chini ya kilo 227 (Qulla mbili), basi taka yoyote inayanajisi maji, iwe imebadilisha moja ya sifa zake au laa. Lakini ikiwa maji yana kilo 227, hayanajisiki mpaka ibadilike mojawapo kati ya sifa zake hizo tatu.

[6] ‘Abdullaah bin ‘Umar alikuwa miongoni mwa wenye kuipa nyongo dunia na mwenye elimu kubwa sana. Alisilimu Makkah wakati akingali kijana mdogo na akahamia Madiynah. Kwanza alishiriki katika vita vya Khandaq, na akafariki mnamo mwaka 73H, akazikwa kule Dhi-Twuwaa.

 

[7] Qulla ni mtungi mkubwa wa udongo unaoweza kuwa na maji yapatayo viriba viwili na nusu, yaani kilo 113.

 

[8] Hii inahusu maji kidogo. Iwapo maji ni mengi, yatahesabika kama maji yanayokwenda au kutiririka, ambayo si machafu na ni mazuri kwa kuogea. Imekatazwa kukojolea maji yaliyosimama ardhini, na kwamba mtu asifanye hivyo ili asizowee kuchafua maji. Maji yanayotiririka kila mara huwa masafi; na hayanajisiki kwa kutiwa takataka au uchafu.

 

[9] Huyu ni mmoja wa Swahaba, na kutokutajwa jina lake hakuiathiri Hadiyth kwa kuwa Swahaba wote walikuwa waaminifu kabisa.

 

[10] Ibn ‘Abbaas: Huyu ndiye ‘Abdullaah bin ‘Abbaas bin ‘Abdul-Mutwalib, binammi wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na Mwanazuoni wa Ummah wa Kiislaam, aliyezaliwa miaka 3 kabla ya Hijrah na akafariki mnamo mwaka 67 A.H.

 

[11] Hadiyth hii inaonekana kama inapingana na ya kwanza, lakini sivyo, kwani amri si ya kukataza moja kwa moja, bali ni mapendekezo ya kukataza ili kuepuka mabaki yoyote ya uchafu.

 

[12] Ieleweke kwamba, kukosha tu uchafu katika chombo, si lazima kuwe mara saba. Falsafa ya kukiosha kitu kikawaida ni tofauti na kukiosha uchafu mahsusi. Madaktari wa zama hizi wanasema kuwa aghalabu katika matumbo ya mbwa huwa kuna viini vya maradhi na minyoo ipatayo urefu wa milimita 4, na hivi hutoka pamoja na kinyesi na hujishikiza kwenye nywele zizungukazo duburi ya mbwa. Mbwa hujisafisha duburi kwa ndimi zao, huchukua viini na minyoo hiyo, na pindi anapolamba chombo au ukimbusu kinywa chake (kama wazungu wafanyavyo). Viini hivi huhamia kwenye chombo au kwenye mdomo wa mtu anayembusu mbwa, na hatimaye huingia tumboni mwa mwana Aadam, na huweza kupenya mpaka kwenye seli za damu na kusababisha magonjwa yanayoweza hata kuua. Kwa kuwa viini hivi havionekani bila darubini. Shariy’ah ya Kiislaam iliamuru kuwa mate ya mbwa kwa ujumla ni najsi, na chochote kinachonajisiwa na mate ya mbwa ni sharti kioshwe mara saba (7), moja ya mara hizi saba, iwe kwa udongo ili kuwa na hakika wa usafi wake. Ili uyajue vyema maudhui haya, tafadhali soma tanbihi chini ya ukurasa wa kitabu cha Ahkaamul-Ahsan, Sharh ’Umdatul Ahkaam.

 

[13] Huyu Abuu Qatada ndiye Al-Haarith bin Rib’I Al Answaar, mwangalizi wa farasi wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Alipigana katika vita vya Uhud, na vita vingine vilivyofuatia. Inasemekana kuwa alifariki Madiynah au Kufa mnamo mwaka 54 A.H.

 

[14] Anas bin Maalik alikuwa mtumishi wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kutoka wakati alipokwenda Madiynah mpaka alipofariki. Anajulikana kwa jina la Abuu Hamzah na alikuwa Mkhazrajiy. Aliishi kule Basra wakati wa ukhalifa wa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ), na akafariki kule akiwa na umri wa miaka 99 au 103, mnamo mwaka wa 91 au 92 au 93 A.H.

 

[15] Hadiyth hii inathibitisha kwamba, mchanga au udongo husafika ukikauka, kama Abuu Shaybah alivyopokea, hususan iwapo utamwagia maji na yatiririke juu ya mahali palipokojolewa.

 

[16] Ni wazi kutoka katika Hadiyth hii kwamba endapo inzi kadondokea katika maji au kinywaji, hakitafanywa kichafu, sawa na viumbe vya familia hii ambayo damu yake haitembei, kama mbu, dondola na buibui, hawakifanyi kinywaji kiwe kichafu wakidondokea au kufia humo.

 

[17] Jina halisi la Abuu Waqiyd ni Al-Haarith bin ‘Awf, na kizazi cha Banu ‘Aamir bin Layth. Alisilimu mapema sana na anahesabika kuwa ni mtu wa Madiynah. Inasemekana kwamba alipigana katika vita vya Badr, aliishi Makkah, na akafariki Makkah mnamo mwaka 65 au 68 A.H alipokuwa na miaka 57, na akazikwa Funj.

 

 

Share