02-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Twahaarah: Mlango Wa Vyombo Vya Chakula, Kunywea Na Kutawadhia

بلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتابُ الطَّهارَة

Kitabu Cha Twahaarah

 

بَابُ الْآنِيَةِ

02-Mlango Wa Vyombo Vya Chakula, Kunywea Na Kutawadhia

 

 

 

 

14.

عَنْ حُذَيْفَةَ بْنِ الْيَمَانِ رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهُمَا، قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ‏{ لَا تَشْرَبُوا فِي آنِيَةِ الذَّهَبِ والْفِضَّةِ، وَلَا تَأْكُلُوا فِي صِحَافِهَا، فَإِنَّهَا لَهُمْ فِي الدُّنْيَا، وَلَكُمْ فِي الْآخِرَةِ } مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Hudhayfah bin Al Yamaaniy[1] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msinywe katika vyombo vya fedha na vya dhahabu na wala msile katika sahani zake[2], kwani hivyo ni vya wasioamini humu duniani na ni vyenu Aakhirah.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

15.

وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهَا، قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ الْلَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{ الَّذِي يَشْرَبُ فِي إِنَاءِ الْفِضَّةِ إِنَّمَا يُجَرْجِرُ فِي بَطْنِهِ نَارَ جَهَنَّمَ } مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ 

Kutoka kwa Ummu Salamah[3] (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika anayekunywa katika vyombo vya fedha anameza moto wa Jahannam tumboni mwake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

16.

وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ الْلَّهِ  صلى الله عليه وسلم ‏{ إِذَا دُبِغَ الْإِهَابُ فَقَدْ طَهُرَ } أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ‏ .‏

 

وَعِنْدَ الْأَرْبَعَةِ: { أَيُّمَا إِهَابٍ دُبِغَ {

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُما) amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ngozi ikitengezwa, imetoharika[4].”   [Imetolewa na Muslim]

 

Na kwa Al-Arba’ah: “Ngozi yoyote iliyotengenezwa.”

 

 

 

17.

وَعَنْ سَلَمَةَ بْنِ الْمُحَبِّقِ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ الْلَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{ دِبَاغُ جُلُودِ الْمَيْتَةِ طُهُورُهاَ } صَحَّحَهُ ابْنُ حِبَّانَ 

Kutoka kwa Salamah bin Al-Muhabbiq[5] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kuisafisha ngozi ya maiti ni kuitakasa kwake.” [Ameisahihisha Ibn Hibbaan]

 

 

18.

وَعَنْ مَيْمُونَةَ رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهَا، قَالَتْ: مَرَّ رَسُولُ الْلَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏بِشَاةٍ يَجُرُّونَهَا، فَقَالَ: {لَوْ أَخَذْتُمْ إِهَابَهَا؟} فَقَالُوا: إِنَّهَا مَيْتَةٌ، فَقَالَ: {يُطَهِّرُهَا الْمَاءُ وَالْقَرَظُ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ

Kutoka kwa Maymuwnah (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipita mbele ya watu wanaoburuza mbuzi akasema: “Lau mgelichukua ngozi yake.” Wakasema: “Huyo ni maiti.” Akasema: “Maji na qaradh huitakasa (ngozi hiyo).” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy]

 

 

19.

وَعَنْ أَبِي ثَعْلَبَةَ الْخُشَنِيِّ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قُلْتُ: يَا رَسُولَ الْلَّهِ، إِنَّا بِأَرْضِ قَوْمٍ أَهْلِ كِتَابٍ، أَفَنَأْكُلُ فِي آنِيَتِهِمْ؟ فَقَالَ: {لَا تَأْكُلُوا فِيهَا، إِلَّا أَنْ لَا تَجِدُوا غَيْرَهَا، فَاغْسِلُوهَا، وَكُلُوا فِيهَا } مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Tha’labah Al-Khushaniyyi[6] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Niliuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Tunaishi katika nchi inayokaliwa na Ahlul-Kitaab. Je tunaweza kula katika vyombo vyao? Akasema: “Msile katika vyombo vyao[7], isipokuwa msipopata vingine, hapo basi viosheni na mle katika vyombo hivyo.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

20.

وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ النَّبِيَّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏وَأَصْحَابَهُ تَوَضَّئُوا مِنْ مَزَادَةِ اِمْرَأَةٍ مُشْرِكَةٍ.‏ مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، فِي حَدِيثٍ طَوِيلٍ

Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn[8] (رضي الله عنهما)  amesema kwamba Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  na Swahaba zake walitawadha kutoka kwenye maji ya kiriba cha ngozi[9] cha mwanamke mshirikina.” [Al-Bukhaariy, Muslim] [Hii ni sehemu ya Hadiyth ndefu]

 

 

21.

وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ ‏ رضى الله عنه ‏ أَنَّ قَدَحَ النَّبِيِّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏اِنْكَسَرَ، فَاتَّخَذَ مَكَانَ الشَّعْبِ سِلْسِلَةً مِنْ فِضَّةٍ.‏ أَخْرَجَهُ الْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kwamba: “Jagi la Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)  lilivunjika, akaziba penye mwanya kwa mnyororo wa fedha.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

[1] Hudhayfah alipewa jina la utani la Abuu ‘Abdillaah. Yeye na baba yake walikuwa Swahaba. Alikuja kuwa maarufu kwa kuwa msiri wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Alifariki Midian (Madain) siku arubaini baada ya kuuliwa ‘Uthmaan katika mwaka wa 35 au 36.H.

 

[2] Hadiyth hii imetajwa hapa kwa madhumuni kuwa, iwapo imekatazwa kunywa au kula kwenye vifaa vya metali hizo, basi kutawadhia vyombo vya metali hizo kumekatazwa, vinginevyo Hadiyth hii ingewekwa katika Mlango wa Kula na Kunywa. Lakini kula na kunywa katika vifaa vilivyopambwa na almasi na rubi inaruhusiwa.

 

[3] Ummu Salamah ni Hindi bint Abiy ‘Umaiyyah. Aliolewa na Abuu Salamah, akahajiri naye hadi Uhabeshi (Ethiopia), na akaja naye hadi Madiynah. Abuu Salamah alipofariki kutokana na jeraha alilolipata katika vita vya Uhud, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuoa mnamo Shawwaal mwaka 4 A.H. Yasemekana kuwa alifariki mwaka 59 au 62 A.H akiwa na umri wa miaka 84, na akazikwa Al-Baqi’.

 

[4] Hadiyth hii inathibitisha kuwa ngozi ikishapitia kwa ufundi wa kiwandani (tasnia), huwa inakuwa safi na nadhifu, inaweza kuwa ni ngozi ya mnyama aliye haraam au halaal kuliwa, na kama mnyama huyo alichinjwa au amekufa mwenyewe. Lakini ngozi za wana Aadam na baadhi ya wanyama ni haraam na haziruhusiwi kutumika. Ngozi ya mwana Aadam ni haraam kwa sababu ya utukufu wake. Na ngozi za wanyama kama mbwa au nguruwe ni haraam kwa sababu wamezaliwa najisi na wachafu. Sharti ikumbukwe kwamba nywele, meno na pembe za wanyama walioruhusiwa pia ni halaal kutumika na kwa biashara.

 

[5] Salamah alipewa jina la utani la Abuu Sinaan wa kabila la Hudhayl. Alihesabika kuwa ni mkazi wa Basra, na Al-Hasan Al-Basr alipokea Hadiyth hii toka kwake.

 

[6] Abuu Tha’labah ni Swahaba aliyetokana na kizazi cha Khushayn bin An-Nimir wa kabila la Quda’a. Alikuwa mmoja wa Swahaba wa Asw-haab Ash-Shajarah waliombai Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) siku ya Al-Hudaibiyyah. Alitumwa kwa watu wake na wote wakasilimu. Aliishi Shaam na akafariki kule mwaka 75 A.H.

 

[7] Hadiyth hii inaweka wazi kuwa, endapo vipo vyombo vya Muislaam, basi visitumike vya asiye Muislaam kwa kula, kupikia chakula, wala kunywea vinywaji. Iwapo kuna uhakika kuwa asiye Muislaam havitumii vyombo vile kwa kula au kunywa vitu haraam, basi vyombo vyake hivyo vinaweza kutumika; lakini hata hivyo sharti kuwa na tahadhari.

 

[8] ‘Imraan alipewa jina la utani la Abuu Nujayd, na anatoka katika kabila la Khuza’a. alisilimu mnamo mwaka wa Khaybar. Alilelewa na kuishi Basra, na akafia hapo mnamo mwaka 52 au 53 A.H.

 

[9] Hadiyth hii inaweka wazi kuwa, vyombo kama hivyo vya waabuduo miungu wengi, vinaweza kutumika bila kusita, kukiwa hakuna uwezekano wa vyombo hivyo kuwa si visafi.

 

 

 

 

Share