Nyama Ng'ombe Ya Kuchoma Na Viazi

Nyama Ng'ombe Ya Kuchoma Na Viazi

Vipimo

  
Nyama ya ng'ombe ya mafupa bila ya

kukatwa (pande kubwa)  -  5- 6 LB (au kiasi unachotaka)

Viazi vilivyomenywa na kukatwa duara  - 4 vikubwa

Kitunguu saumu/thomu na tangawizi iliyosagwa - 2  Vijiko vya supu

Pilipili mbichi iliyosagwa  - 1 Kijiko cha supu

Mtindi (Yoghurt) - 1 Kijiko cha supu

Pilipili manga ya unga - 2 vijiko vya chai 

Bizari ya pilau ya unga

(Jiyra/cummin powder) - 2 vijiko vya chai

Siki - 4 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika 

  1. Changanya thomu, tangawizi, chumvi, pilipili manga, pilipili mbichi, mtindi, bizari ya pilau, na siki katika kibakuli kidogo.
  2. Ichanje chanje nyama upate kuingiza mchanganyiko huo wa masala, kisha tia kidogo kidogo katika hizo sehemu wazi katika nyama na uroweke pande la nyama kwa muda  wa nusu saa.
  3. Liweke katika trea ya kupikia ndani ya jiko (oven). Ifunike kwa jaribosi ya kupikia (foil paper) na ipike katika moto mkali 400º- 450º kwa muda wa saa au zaidi. Inategemea ukubwa wa nyama, ikiwa ni pande kubwa sana zidisha muda wa kupikia.
  4. Karibu na kuwiva, vitie viazi chumvi na pilipili manga kidogo na  umwagie juu ya nayma na uendelee kupika hadi viazi viwive pia.
  5. Epua ikiwa tayari kuliwa. 

Kidokezo:  Nzuri kuliwa na mikate 'Pita pan bread, (au mikate ya kiarabu) saladi na hummus (sosi ya ufuta na dengu zilizosagwa). (Au sosi ya shawarma)    

 

 

 

Share