007-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Vyakula Na Vinywaji: Damu Ya Mnyama Aliyechinjwa

 

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الأَطْعِمَةِ وَالأَشْرِبةِ وَمَا يَتَعَلَّقُ بِهِمَا

 

 Kitabu Cha Vyakula Na Vinywaji Na Yanayohusiana Na Viwili Hivi

 

Alhidaaya.com

 

 

007- Vilivyoharamishwa Na Kitabu Cha Allaah: 

Damu Ya Mnyama Aliyechinjwa (02)

 

 

 

2-  Damu Ya Mnyama Aliyechinjwa

 

Si halali kula au kunywa damu ya mnyama aliyechinjwa.  Ni kwa Neno Lake Ta’aalaa:

 

"حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةُ وَالدَّمُ"

 

“Mmeharamishiwa nyamafu, na damu”.  [Al-Maaidah: 03].

 

Ama damu kidogo kama ile inayobaki ndani ya mishipa ya mnyama aliyechinjwa ambayo ni vigumu kuepukana nayo, damu hii inasamehewa.

 

 

·        Damu Iliyo Nje Ya Duara La Uharamu

 

Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

" أُحِلَّتْ لَنَا مَيْتَتَانِ وَدَمَانِ: ...... وَأَمَّا الدَّمَانِ: فالْكَبِدُ وَالطِّحَالُ "

 

“Tumehalalishiwa maiti mbili na damu mbili… na ama damu mbili, basi ni ini na wengu.  [Hadiyth Swahiyh.  Imepita nyuma kidogo].

 

 

 

Share