023-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Vyakula Na Vinywaji: Watu Wale Kwa Pamoja Na Mtu Asile Peke Yake

 

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الأَطْعِمَةِ وَالأَشْرِبةِ وَمَا يَتَعَلَّقُ بِهِمَا

 

Kitabu Cha Vyakula Na Vinywaji Na Yanayohusiana Na Viwili Hivi

 

Alhidaaya.com

 

Adabu Za Kula

 

023-Watu Wale Kwa Pamoja Na Mtu Asile Peke Yake

 

 

 

 

7-  Watu Wale Kwa Pamoja Na Mtu Asile Peke Yake

 

 

 

Kwa kuwa mikono mingi kwenye chakula hukiongezea baraka kama alivyosema Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

"طَعَامُ الاِثْنَيْنِ كَافِي الثَّلاَثَةِ وَطَعَامُ الثَّلاَثَةِ كَافِي الأَرْبَعَةِ‏"

 

“Chakula cha wawili huwatosha watatu, na chakula cha watatu huwatosha wanne”.  [Hadiyth Swahiyh.  Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (5392) na Muslim (2058)].

 

Imesimuliwa kwamba Maswahaba wa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) walisema: 

 

 

"يَا رَسُوْلَ اللهِ ، إِنَّا نَأْكُلُ وَلاَ نَشْبَعُ ، فَقَالَ : فَلَعَلَّكُمْ تَفْتَرِقُوْنَ؟ قَالُوْا  نَعَمْ ، قَالَ : فَاحْتَمِعُوْا عَلَى طَعَامِكُمْ ، وَذْكُرُوا اسْمَ الله ، يُبَارِكْ لَكُمْ فِيْهِ"

 

“Ee Rasuli wa Allaah!  Mbona sisi tunakula na wala hatushibi?! Rasuli akawaambia:  Huenda nyinyi mnakula kila mmoja kivyake.  Wakasema: Ni kweli.  Akasema:  Basi jumuikeni pamoja katika chakula chenu, na litajeni Jina la Allaah, na Yeye Atawabarikieni ndani yake”.  Hadiyth hii ni Dhwa’iyf.

 

 

Share