09-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume: Haki Zinazompasa Mke Kumtendea Mumewe: 8-Amlinde Kwa Kujichunga Yeye Mwenyewe, Watoto Wa Mumewe Na Mali Yake

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الزَّوَاجِ

 

Kitabu Cha Ndoa

 

الحُقُوْقُ بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ

 

Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume

 

Alhidaaya.com

 

 

08:  Haki Zinazompasa Mke Kumtendea Mumewe: 8-Amlinde Kwa Kujichunga Yeye Mwenyewe, Watoto Wa Mumewe Na Mali Yake:

 

Allaah Ta’alaa Amesema:

 

"فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ"

 

Basi wanawake wema ni wale watiifu wenye kujihifadhi katika hali ya kutokuweko waume zao kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajihifadhi.  [An-Nisaa: 34]

 

At-Twabariy akiifasiri aayah hii amesema:  “Yaani, wanajihifadhi wenyewe wakati waume zao wanapokuwa hawapo, kwa kuzilinda tupu zao na mali za waume zao”. 

 

Nyuma tumeitaja Hadiyth hii isemayo kuhusu mwanamke bora zaidi isemayo:

 

"الَّتي تُطيْعُ زَوْجَهَا إِذَا أَمَرَ، وَتَسُرُّهُ إِذَا نَظَرَ، وَتَحْفَظُهُ فِي نَفْسِهَا وَمَالِهِ"

“Ni yule anayemsikiliza mumewe anapomwamrisha, anamfurahisha anapomtazama, na anamlinda kwa kujichunga yeye mwenyewe na mali ya mumewe”.  [Hadiyth Swahiyh.  An-Nasaaiy (6/68)]

 

 

Share