Chow Mein (Tambi Nene Za Kukaanga) Za Nyama Kusaga Na Mboga Mchanganyiko

Chow Mein  (Tambi Nene Za Kukaanga) Za Nyama Kusaga Na Mboga Mchanganyiko 

 

 

Vipimo

 

Noodles (Tambi nene  za tayari) - 1 paketi (500 gm)

Nyama ya kusaga - 1 Lb

Mafuta ya ufuta (Sesame oil) - 3 vijiko vya supu

Njegere changa (Spring onions) - ½  kikombe

Karoti ilokatwakatwa - ½ kikombe

Mahindi - ½ kikombe

Maharage mabichi ya kijani -  ½ kikombe

Sosi ya soya (soy sauce) - 3 vijiko vya supu

Sosi ya nyanya/Tomato ketchup - 3 vijiko vya supu

Kitunguu saumu(thomu/galic) ilokunwa (grated) - 5 - 7 chembe

Tangawizi mbichi ilokunwa (grated) - 1 kipande

Pilipili manga - ½ kijiko cha chai

Paprika au pilipili nyekundu -  ½ kijiko cha chai

Chumvi - kiasi

Maji -  ½ kikombe

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

 

1. Chambua noodles (tambi nene). Ikiwa ni zilozongoreka zikatekate kama kwenye picha.

2. Chemsha maji na zipike kama inavyoelezwa katika paketi. Au chemsha kiasi ya dakika chache tu zisiive sana hadi zikawa laini sana. Chuja maji. Changanya na siagi ili zisigandane.

3. Weka mafuta katika kisufuria kisha tia kitunguu thomu na tangawizi , kaanga harakaharaka kidogo tu kisha tia sosi zote, endelea kukaanga kidogo tu.

4. Tia nyama ya kusaga  kaanga.

5. Tia mboga zote, na maji kisha funika mboga ziive.  

6. Katika bakuli kubwa mimini tambi kisha changanya pamoja na sosi ya nyama ya kusaga ikiwa tayari.

Kidokezo:

Sio lazima kupatikana tambi za aina hiyo ya paketi. Muhimu ni tambi zozote nene (noodles)

 

 

Share