Kusafirisha Maiti Japo Kuna Waislamu, Kuipeleka Alipotoka Inajuzu?

 

Kusafirisha Maiti Japo Kuna Waislamu, Kuipeleka Alipotoka  Inajuzu?

 

Alhidaaya.com

 

Swali:

 

Assalam Alykum wa -Rahmatu Allaahi wa barakatuh. ALLAAH akujaliyeni kila la kheri na afya njema. Nina shukuru kwa msaada wenu na kwakujitolea kutu elimisha.

 

Swali langu nikuomba kuelimishwa mimi na wenzangu kuhusu maisha tunao kwa wakazi wa europa. Je, ni halali kusafirisha maiti, ikiwa kuna waislam hapo?

 

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Haijapatikana kabisa katika historia na maisha ya Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi  wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu ‘anhum) kuwa walisafirisha maiti ili kwenda kuzikwa sehemu nyingine.

 

Hivyo, haijuzu kwa Muislamu kusafirisha maiti ya Muislamu kuipeleka sehemu nyingine ili ipate kuzikwa. Ni jukumu la Waislamu wa sehemu hiyo kumfanyia mambo manne maiti huyo, nayo ni:

 

1.   Kumuosha.

 

2.   Kumkafini.

 

3.   Kumswalia.

 

4.   Kumzika.

 

Wale ambao si katika jamaa zake wafanye bidii kumuombea maghfira kwa Allaah Aliyetukuka.

 

Tafadhali bonyeza kiungo kifuatacho upate maelezo zaidi:

 

Inafaa Kusafirisha Maiti Kutoka Mji Hadi Mji Mwengine?

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share