Skip to main content

 Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com

25-Je, Inajuzu kutufu makaburi?

Hapana! Haijuzukutufu (kuzunguka) makaburi, bali kutufu ni kwa ajili ya Ka'abah pekee.

 وَلْيَطَّوَّفُوا بِالْبَيْتِ الْعَتِيقِ ﴿٢٩﴾

Na watufu kwenye Nyumba ya Kale. (Al-Ka’bah) [Al-Hajj: 29]

((مَنْ طافَ بِالْبَيْتِ سَبْعاً وَصَلّى رَكَعَتينِ كَانَ كَعتق رَقَبة))  رواه ابن ماجه و صححه الألباني 

((Atakayezunguka Ka'bah mara saba kisha akaswali rakaa mbili ni kama mfano kamwacha huru mtumwa mmoja)) [Ibn Maajah na ameisahihisha Al-Albaniy katika Swahiyh Al-Jaami’ (6379)]