Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Hakuna Dalili Ya Khatwiyb Kusoma Aayah Zinazohusiana Na Maudhui Ya Khutbah
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn
Hakuna Dalili Ya Khatwiyb Wa Ijumaa Kusoma
Aayah Zinazohusiana Na Maudhui Ya Khutbah
Imaam Muhammad bin Swaalih Al-'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)
Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:
"...Lakini hapa kuna mas-alah (ambayo) baadhi ya Maimaam wanayafanya, (nayo ni) pindi (Khatwiyb) anapokhutubu, husoma ndani ya Swalaah zile Aayaat zenye mnasaba nayo (khutbah); hili husemwa kuwa ni bid'ah.
Kwa hakika si vinginevyo, Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akijilazimu kwa kusoma Sabbihisma na Al-Ghaashiyah. Au akisoma (Suwrat) Al-Jumu'ah na Al-Munaafiquwn. Na wala hakuwa akichunga (kusoma Aayah) zenye kuhusiana na maudhui ya khutbah.
[Liqaat Al-Baab Al-Maftuwh, mj. 18, uk. 155]