Fataawaa: Mukhtasari Wa Fataawaa Kuhusu Yanayobatilisha Na Yasiyobatilisha Swawm

 

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

Yafuatazo Ni Mukhtasari Wa Mas-alah Ambayo Aghlabu Huulizwa Khaswa Katika Ramadhwaan Kuhusiana Na Swawm

 

 

1-At-Tahaamiyl: (Suppository) Dawa Za Kuteremsha Homa Zinazowekwa Kwa Njia Ya Utupu Wa Nyuma

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Imaam ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

2-Dawa Ya Macho Ya Maji (Eye Drops)

 

Hukmu Yake: Haibatilishi. Lakini atakapohisi ladha ya hiyo dawa kwenye koo lake, basi kiakiba akilipa hiyo siku ni bora.

 

[Imaam Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

 

3-Wanja Wa Macho

 

Hukmu Yake: Haibatilishi na lakini ni bora atumie usiku baada ya kufuturu.

 

 [Ibn ‘Uthaymiyn, Ibn Baaz]

 

 

 

4-Dawa Ya Kudondoshea Masikioni

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

5-Kipulizo Cha Pumu.

 

Hukmu Yake:  Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn, Al-Lajnah Ad-Daaimah]

 

 

 

6-Kipulizo; Mashine Ya Kuvuta Hewa (Oxygen)

 

Hukmu Yake: Haibatilishi kwa kuhitajika kwa dharura.

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

7-Sindano Ya Penicillin

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

8-Sindano Ya Insoline Kwa Mgonjwa Wa Kisukari

 

Hukmu Yake:  Haibatilishi.

 

 [Ibn ‘Uthaymiyn, Ibn Baaz]

 

 

 

 

9-Sindano Ya Ganzi Kwa Ajili Ya Kung’olewa Jino Na Kuweka Mjazo Wa Meno Na Kusafishwa Meno

 

Hukmu Yake: Haibatilishi. Lakini atahadhari kumeza chochote katika dawa na damu (kwa maana akimeza atabatilisha Swawm).

 

[Ibn Baaz]

 

 

 

10-Kutumia Manukato Mazuri Na Kuyanusa

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

11-Kunusa Harufu Ya Udi Uliofukizwa

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

12-Dawa Ya Kulainisha Mdomo (Lip Balm)

 

Hukmu Yake: Haibatilishi, kwa sharti kwamba asimeze kitu.

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

13-Vipodozi (Make Up)

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

Tanbihi: Mwanamke hapaswi kujipamba kudhihirisha mapambo yake kwa wanaume ajnabiy wasio mahaarim wake.

 

 

 

 

14- Kuvuja Damu Pua Na Kun’goa Jino Huku Damu Ikitoka

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

15-Kutolewa Damu Kwa Ajili Ya Kipimo

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

16-Kuota Kitendo Cha Ndoa Na Kutokwa Manii

 

Hukmu Yake: Haibatilishi

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

 

17-Kutokwa Na Madhii. (Madhii Ni Maji Mepesi Mno Yenye Kunatanata Yanayotoka Wakati Wa Matamanio Ya Kimwili)

 

Hukmu Yake: Haibatilishi

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

18-Kuogelea Na Kupiga Mbizi

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

19-Dawa Ya Kusukutua

 

Hukmu Yake: Haibatilishi kwa sharti kuwa asimeze kitu.

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

20-Kutumia Mswaki

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

Lakini ni mswaki wa kawaida na si ambao una ladha.

 

 

 

 

21-Dawa Ya Kusafisha Meno

 

Hukmu Yake: Haibatilishi ikiwa haitomezwa ikaingia tumboni. Na lililo salama zaidi ni kutokuitumia kwa sababu ina nguvu kali.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

22-Kumeza Makohozi

 

Hukmu Yake: Haibatilishi ikiwa haitofikia mdomoni. Ama ikifikia mdomoni akameza, basi inabatilisha Swawm.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

23-Kuonja Chakula

 

Hukmu Yake: Haibatilishi lakini bila ya kumeza na wala asifanye mtu isipokuwa kwa dharura.

 

 [Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

24-Vidonge Vinavyoweka Chini Ya Ulimi Kwa Kutibu Maradhi Ya Moyo

 

Hukmu Yake: Haibatilishi ikiwa havitoyeyuka na kumezwa mate yake ambayo yameyeyuka ndani ya mdomo. Hakika vinabatilisha Swawm. Lakini vikiwa haviyeyuki na havimezwi, basi havina madhara.

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

25-Dawa Ya Kudondoshea Puani

 

Hukmu Yake: Inabatilisha ikifikia tumboni [akimeza].

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

Dawa ya pua haifai kwa mwenye Swawm na atakayetia ikafikia kooni akasikia ladha yake, basi alipe Swawm yake.

 

 

 

 

26-Viraka Vya Nikotini (Vya Kubandika Mikononi Au Mabegani Kusaidia Wavutaji Sigara Waache Uvutaji)

 

Hukmu Yake: Inabatilisha.

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah]

 

 

 

 

27-Hijaamah (Kupigwa Chuku, Kuumikwa)

 

Hukmu Yake: Inabatilisha.

(Lakini Wanachuoni wengine wanaonelea ikiwa haitomdhoofisha anayefanyiwa Hijaamah, basi haibatilishi).

 

 [Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

28-Kuchangia Damu

 

Hukmu Yake: Inabatilisha ikiwa ni nyingi (na kumdhoofisha mtoaji damu) kama vile kiasi cha damu ya Hijaamah.

 

 [Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

29-Damu Inayotoka Katika Kidonda

 

Hukmu Yake: Inabatilisha ikiwa si kwa khiari yake kama vile kutolewa damu nyingi kwenye mishipa kwa ajili ya vipimo, lakini ikiwa ni kwa dharura bila ya khiari yake basi haibatilishi.

 

 

 

 

30-Kutapika Kwa Makusudi

 

Hukmu Yake: Inabatilisha ikiwa kwa makusudi. Ikiwa si makusudi haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

31-Sindano Ya Kuingiza Chakula Kupitia Maji Mwilini Kumtia Mtu Nguvu

 

Hukmu Yake: Inabatilisha.

 

Ama sindano ya misuli au ya mishipa au ya ngozi haibatilishi. Na ni salama zaidi kufanya usiku baada ya kufuturu.

 

[Ibn ‘Uthaymin, Ibn Baaz]

 

 

 

32-Kuvuta Harufu Ya Moshi Wa Udi

 

Hukmu Yake: Inabatilisha ikiwa anajua, ama ikiwa kunusa tu haibatilishi.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

33-Kujichua (Masturbation)

 

Hukmu Yake: Haijuzu katika Ramadhwaan wala nje ya Ramadhawaan na inabatilisha Swawm.

 

[Ibn Baaz, Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

 

34-Kudungwa Sindano

 

Hukmu Yake: Haibatilishi. Ama ikiwa ni kwa ajili ya kuingiza chakula au nguvu ya chakula (kama glucose) inabatilisha. Na usalama zaidi kutumia usiku [baada ya kufuturu].

 

[Ibn Baaz]

 

 

 

35-Kupaka Hinna

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

36-Kula Au Kunywa Kwa Kusahau

 

Hukmu Yake: Haibatilishi, lakini mtu anapokumbuka tu aachilie mbali hata kama kimo mdomoni akiteme.

 

[Ibn ‘Uthayimyn].

 

 

 

37-Kuvuta Sigara

 

Hukmu Yake: Inabatilisha na ni haramu wakati wowote katika Ramadhwaan na nje ya Ramadhwaan.

 

[‘Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

38-Kuoga

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

39-Kumeza Chakula Kilichokuja Kwa Kucheua

 

Hukmu Yake: Inabatilisha ikiwa chakula au maji aliyocheua yatafika mdomoni akameza, ama ikiwa yameishia kooni basi hana juu yake chochote

 

[Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

40-Kusafishwa Damu Ya Mafigo (Dialysis)

 

Hukmu Yake: Inabatilisha na inampasa alipe Swawm yake.

 

[Ibn Baaz]

 

 

 

41-Maongezi Maovu Ya Haramu

 

Hukmu Yake:  Hayabatilishi lakini thawabu zitapunguka  na kama yanahusiana na haki ya mtu (Kumtusi mtu), basi itampotezea kabisa thawabu za Swawm.

 

[Ibn Baaz]

 

 

 

42-Kumeza Mate

 

Hukmu Yake: Haibatilishi.

 

[Ibn Baaz]

 

 

 

43-Kumeza Maji Wakati Wa Wudhuu

 

Hukmu Yake: Haibatilishi ikiwa si kwa kukusudia.

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah]

 

Share