SWALI:
Asalam Aleikum WarahmatuLlahi wabarakatu, Naomba nifahamishwe vizuri kuhusu kureje kwa Nabii Issa (Aleihi Salaam). Kuna mambo ambayo yanayotatiza kuhusu kurejea kwake. Kwanza Nabii Issa alitumwa na Allaah kwa Umma wa Banii Israil ambao walimkataa na kukufuru na alikuja na injili ambayo wakristo wametengeneza
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kurudi kwa Nabii ‘Iysa (‘alayhis Salaam).
Sisi Waislamu hatuna shida, tatizo wala utata kuhusiana na Nabii ‘Iysa (‘alayhis Salaam) kwani Allaah Aliyetukuka na Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wametuelezea kila kitu kuhusu yeye, kuanzia kuzaliwa kwake, utoto wake, kupazwa kwake mbinguni pasi na kuuliwa na Mayahudi na pia kurudi kwake.
Mayahudi na Wakristo wana
Hili ni suala muhimu la kiimani na jambo la kuamini ghaibu. Na kuamini mambo ya ghaibu ni katika mambo ya Ki-Itikadi na Imani. Allaah Aliyetukuka Amewasifu wale wenye kuamini ya ghaibu kwa kusema:
“Ambao huyaamini ya ghaibu na husimamisha Swalah, na hutoa katika tuliyowapa. Na ambao wanayaamini yaliyoteremshwa kwako, na yaliyoteremshwa kabla yako; na Akhera wana yakini nayo” (al-Baqarah [2]: 3 – 4).
Bonyeza upate manufaa zaidi:
Nabii ‘Iysa Atakua Katika Kundi Gani Miongoni Mwa Makundi 72?
Nabii ‘Iysa Ametabiriwa Katika Qur-aan Kuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)?
Nani Aliyesulubiwa Badala ya Nabii 'Iysa ('Alayhis Salaam)?
Nini Ukweli Kuhusu Kupandishwa Nabii 'Iysa عليه السلام
Na Allaah Anajua zaidi