Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Iyd: Hukmu Ya Wanaume Kukumbatiana Siku Ya 'Iyd, Na Hukmu Ya Kuwabusu Wanawake Walio Maharimu

Iyd: Hukmu Ya Wanaume Kukumbatiana Siku Ya 'Iyd,

Na Hukmu Ya Kuwabusu Wanawake Walio Maharimu

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

 Alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Ni ipi hukmu ya Wanaume kukumbatiana Siku ya 'Iyd, na kuwabusu Wanawake ambao ni Maharimu?

 

 

 

JIBU:

 

 

Na yale wayafanyayo watu Siku ya 'Iyd kwa Wanaume kukumbatiana, hili halina tatizo ndani yake.

 

Na kuwabusu Wanawake ambao ni Maharimu (ndugu wa damu au wale ambao ni haramu kuwaoa), hakuna ubaya kwa hilo, lakini Wanachuoni wamesema ni karaha (Makruuh) isipokuwa mama, atabusiwa kwenye kichwa chake au kwenye kipaji chake. Na hivyo hivyo (inaruhusiwa) kwa bint na Maharimu wengine.

 

Iepukwe kuwabusu mashavuni. Hilo ni salama zaidi.

 

 

[Majmuw' Fataawa wa Rasaail Ash-Shaykh Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah), Mj.16, uk. 222]

 

 

 

Share