Bin-Aadam Anatokana Na Kizazi Cha Nyani?

 

Bin-Aadam Anatokana Na Kizazi Cha Nyani?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Pia ninahitaji kufahamu, tunasoma kuwa Binadamu ametokana na generation ya nyani? je Qur'aan inasemaje ya suala hili.

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

Hakika nadharia hiyo haina ithbati yoyote kutoka hata kwa sayansi yenyewe. Bali nadharia hiyo ililetwa na Myahudi Darwin ili kumdhalilisha mwanaadamu. Nadharia hiyo ni potofu na ni kinyume na Qur-aan.

 

Hiyo ni kuwa Allaah Aliyetukuka Anatuambia:

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ ﴿٤﴾

Kwa yakini Tumemuumba mwana-Aadam katika umbile bora kabisa. [At-Twiyn 95: 4].

 

Na Akasema:

الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ ﴿٧﴾

Ambaye Amekuumba Akakusawazisha (umbo sura, viungo) na Akakupima na kukulinganisha sawa. [Al-Infitwaar: 7].

 

Na Aayah zinazotueleza kuwa mwanaadamu ameumbwa na Allaah Aliyetukuka ni nyingi sana.

 

Kadhalika hakuna Muislam asiyefahamu kuwa Aadam (‘Alayhis-salaam) ambaye ni mwanaadam wa kwanza, aliumbwa kwa udongo na akatokana naye mkewe Hawwaa na vizazi Haabiyl na Qaabiyl hadi kutufikia sisi leo hii. Sasa huyo nyani katokea wapi hapo?

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share