Kuku Kidari Kwa Sosi Ya Malai

Kuku Kidari Kwa Sosi Ya Malai

 

 

 

Mahitajio

Utayarishaji

Kipimo

 

Kuku bila ya mfupa (kidari)

katakata osha

1 kilo

Kitunguu maji

katakata (chop)

2

Tungule/nyanya

    “

2

pilipili mbichi/shamba kijani

Saga

3

Kitunguu thomu/saumu

katakata (chop)

7-10 chembe

Tangawizi mbichi

saga

1 kipande

chumvi

 

kiasi

Pilipili nyekundu ya unga

 

1 kijiko cha chai

Malai (cream)

tumia ya tayari

1 gilasi

Bizari pilau/ jiyrah/cummin

 

1 kijiko cha chai

Gilgilani/Dania/corriander

 

1 kijiko cha chai

Mafuta

 

1/3 kikombe

 

Namna Ya Kupika:

  1. Weka mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu maji hadi vilainike- Usiache mpaka vikageuka rangi sana.
  2. Tia kitunguu thomu/saumu na tangawizi mbichi endelea kukaanga.
  3. Tia vipande vya kuku, endelea kukaanga kidogo
  4. Tia nyanya, bizari zote, chumvi, pilipili mbichi endelea kukaanga
  5. Mwishowe tia malai , changanya vizuri, acha ichemke kidogo kuku aive.
  6. Ongezea malai mwishoni baada ya kuzima moto, changanya vizuri, epua.

 

 

 

 

 

Share